Endelea Mbele (Bwana Atakupigania, Nawe Utanyamaza Kimya)
“Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu,
mkauone wokovu wa BWANA atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo
hamtawaona tena milele. BWANA ATAWAPIGANIA NINYI, NANYI MTANYAMAZA KIMYA. BWANA
akamwambia Musa, Mbona unanililia mimi? WAAMBIE WANA WA ISRAELI WAENDELEE
MBELE.” Kutoka 14: 13-15
Bwana Yesu Kristo asifiwe milele!
Namshukuru Mungu sana kwa kutupa neema ya kumtumikia
siku nyingine nzuri ya leo. Rehema na fadhili zake ni nyingi mno katika maisha
yetu. Ni rehema zake tu kwamba hatuangamii na fadhili zake ni mpya kila siku
asubuhi.
Leo nimetumwa kukuhamasisha wewe ambaye unapita
katika kipindi kigumu kwenye maisha yako. Wewe ambaye mbele yako unaona bahari
ya shamu na akili zako zimefika mwisho na huoni mpenyo wa kutokea hapo
unapopita. Nimetumwa leo nikutie moyo na kukukumbusha kuwa Mungu amehaidi
atakupigania nawe utanyamaza kimya.
Wana wa Israeli walifika sehemu wakapata hofu kuu
pale ambapo walikutana na bahari ya shamu mbele yao na nyuma yao kulikuwa na
jeshi kubwa na la kutisha la Wamisri. Walifika sehemu wakakata tamaa kabisa na
kuona huo ndio mwisho wao na hakuna tena tumaini mbele yao.
Lakini tunamuona mtumishi wa Mungu, Musa akiwatia
moyo na kuwaambia wasiogope, wasimame tu, wakauone wokovu wa Bwana atakaofanya;
kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele. Bwana atawapigania
ninyi, nanyi mtanyamaza kimya.
Wewe ambaye unapita mahali pagumu sikia Neno la Bwana;
USIOGOPE, SIMAMA KIUME TU, UKAUONE WOKOVU WA BWANA ATAKAOFANYA; KWA MAANA HAO
WAMISRI( MAHALI PAGUMU UNAPOPITIA, ILO JARIBU, HIYO SHIDA, HIYO HOFU KUU) HAUTAIONA TENA MILELE. BWANA ATAKUPIGANIA
WEWE, NAWE UTANYAMAZA KIMYA.
Mungu anakwambia endelea mbele tu, endelea mbele,
usikate tamaa. Ndio anajua mbele yako kuna bahari ya shamu, ndio anajua mbele
yako kuna jaribu. Unapoona huoni mwisho wake na inawezekana umekaa hapo muda
mrefu na umeshindwa kutoka. Akili zimegoma, hakuna anayekupa msaada, marafiki
na ndugu wamekukimbia. Lakini Bwana anasema ENDELEA MBELE, USIKATE TAMAA,
NITAIPASUA HIYO BAHARI YA SHAMU NA WEWE UTAPITA SALAMA.
Mungu anataka uchukue hatua ya imani ya kuendelea
mbele bila woga wala hofu, ukimwamini kwamba hiyo bahari sio kitu
kinachomshinda Yeye. Anaweza akakupitisha kwenye hiyo bahari kama tu utamwamini
Yeye.
Mungu amehaidi atafanya mlango wa kutokea kwenye ilo
jaribu. Mwamini Mungu na uendelee mbele, usikate tamaa, Yeye amehaidi kukutetea
na kukusadia. USIRUDI NYUMA, ENDELEA MBELE KWA IMANI.
“Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida
ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; amabye hatwaacha mjaribiwe kupita
mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu ATAFANYA NA MLANGO WA KUTOKEA, ili mweze
kustahimili.” 1 Wakorintho 10:13
“Usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe;
usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; NITAKUTIA NGUVU, NAAM, NITAKUSAIDIA,
naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.” Isaya 41:10
Nikomee hapa kwa leo. Baraka na wema wa Bwana viwe
pamoja nawe sasa na hata milele. AMEN.
YESU ANAKUPENDA WEWE AMBAYE HUJAMPA MAISHA YAKO. UFALME
WA MUNGU UMEKARIBIA SANA. UNASUBIRI NINI KUMPOKEA YESU NA KUMTUMIKIA? WAKATI
NI SASA. MPOKEE YESU AWE BWANA NA
MWOKOZI WA MAISHA YAKO LEO.
“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata
akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa
milele.” Yohana 3:16
Usikubali kupotea kwa kutokumwamani Yesu. Fanya maamuzi
muhimu leo ya kumpokea Yesu, kwa sababu YESU NI NJIA, KWELI NA UZIMA (Yohana
14:6)
Maoni