Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2017

Mbona Basi Mnaifanya Migumu Mioyo Yenu?

Picha
“Mbona, basi mnaifanya migumu mioyo yenu, kama vile wale Wamisri, naye yule Farao, walivyoifanya mioyo yao?...” 1Samweli 6:6 Bwana Yesu Kristo asifiwe! Ni jambo jema kumshukuru Mungu kwa kutupa kibali tena cha kuiona siku hii nyingine na wiki nyingine tena ya leo. Namshukuru mungu kwa wema na fadhili zake zinazotufuata siku zote za maisha yetu kila iitwapo leo. Leo ningependa kuongea na wewe ambaye umekuwa unafanya moyo wako kuwa mgumu na hutaki kuisikia sauti ya Mungu na kumpa Yesu maisha yako. Naongea pia na wewe ambaye umeanguka dhambini na umeshindwa kurudi kwa Yesu tena. Mbona unaufanya moyo wako kuwa mgumu? Mbona utaki kuokoka? Nini kinakuzuia kumpa Yesu maisha yako? Je ni mali au shughuli za dunia? Je ni wazazi, ndugu au mpenzi? Je unajiona bado wewe ni mdogo na unasema ngoja nile ujana kwanza, Yesu badae? Je dhambi zimekuzidia unaona kwamba huwezi kuziacha? Sijui sababu yako ni ipi ndugu yangu inayokufanya usimpe Yesu maisha yako. Wakati ni sasa wa kump...

Endelea Mbele (Bwana Atakupigania, Nawe Utanyamaza Kimya)

Picha
“Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa BWANA atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele. BWANA ATAWAPIGANIA NINYI, NANYI MTANYAMAZA KIMYA. BWANA akamwambia Musa, Mbona unanililia mimi? WAAMBIE WANA WA ISRAELI WAENDELEE MBELE.” Kutoka 14: 13-15 Bwana Yesu Kristo asifiwe milele! Namshukuru Mungu sana kwa kutupa neema ya kumtumikia siku nyingine nzuri ya leo. Rehema na fadhili zake ni nyingi mno katika maisha yetu. Ni rehema zake tu kwamba hatuangamii na fadhili zake ni mpya kila siku asubuhi. Leo nimetumwa kukuhamasisha wewe ambaye unapita katika kipindi kigumu kwenye maisha yako. Wewe ambaye mbele yako unaona bahari ya shamu na akili zako zimefika mwisho na huoni mpenyo wa kutokea hapo unapopita. Nimetumwa leo nikutie moyo na kukukumbusha kuwa Mungu amehaidi atakupigania nawe utanyamaza kimya. Wana wa Israeli walifika sehemu wakapata hofu kuu pale ambapo walikutana na bahari ya shamu mbele yao na nyuma y...

Maamuzi Magumu (Wakoma Kishindo Cha Jeshi Kubwa)

“Basi walikuwako watu wanne wenye ukoma, penye lango la mji; wakasemezana, Mbona tunakaa hapa hata tufe? Tukisema, tutaingia mjini, mjini mna njaa, nasi tutakufa humo; nasi tukikaa hapa, tutakufa vile vile. Haya! Twende tukaliendee jeshi la Washami; wakituhifadhi hai tutaishi; wakituua, tutakufa tu.” 2Wafalme 7: 3-4 Bwana Yesu asifiwe! Namshukuru Mungu kipekee kabisa kwa kutupa neema ya kuiona siku hii mpya ya leo. Ni huruma zake tu kwamba hatuangamii. Fadhili zake ni mpya kila inapoitwa leo. Leo Mungu ametupa tujifunze kuchukua maamuzi magumu. Maamuzi magumu waliyoyachukua wakoma hawa yaliwaokoa wao na Israeli yote kutoka kwenye njaa kali. Kama hawa wakoma wasingefanya maamuzi magumu kwa kuangalia hali walizonazo sijui kama chakula kingepatikana. Walichukua maamuzi ambayo yalihatarisha maisha yao. Walikuwa tayari kupoteza maisha yao kwa sababu walijua hata kama wangebaki pale walipo wangekufa tu. Walichukua maamuzi ya kufa na kupona na kupitia maamuzi yao Israeli yote...